NIGERIA-DRC-SOKA-MICHEZO
Nigeria kumenyana na DRC, katika mechi ya kirafiki
Timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, inachuana na Nigeria siku ya Jumatatu katika mchuano wa Kimataifa wa kirafiki mjini Port Harcourt.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mchuano huu unatarajiwa kuisaidia Nigeria katika maandalizi yake ya kucheza katika fainali ya kombe la dunia nchini Urusi mwezi Juni.
Nigeria imepangwa katika kundi D na Argentina, Iceland na Croatia.
Leopard, inawakilishwa na wachezaji 23 wakiwemo saba, wanaocheza soka ya kulipwa nje ya nchi hiyo.
Mechi nyingine ya Kimataifa ya kirafiki ni kati:-
Kenya vs Equitorial Guinea
Ureno vs Tunisia
Ufaransa vs Jamhuri ya Ireland
Uturuki vs Iran
Italia vs Saudi Arabia