Ufaransa kupepetana na Ujerumani Novemba 14
Timu ya taifa ya soka ya Ufaransa na Ujerumani, zitamenyana mjini Cologne katika mchuano wa Kimataifa wa kirafiki tarehe 14 mwezi Novemba.
Imechapishwa:
Shirikisho la soka nchini Ufaransa limetangaza tarehe hii, na mchuano huo utakuwa ni kama nusu fainali ya kuwania taji la bara Ulaya mwaka 2016, mchuano ambao Ufaransa walishinda kwa mabao 2-0, mabao yote mawili yakifungwa na Antoine Griezmann.
Mchuano huu umetangazwa pia baada yas Ufaransa kufuzu katika fainali ya kombe la dunia mwaka ujao, hapo jana baada ya kusihinda Belarus mabao 2-1.
Ujerumani pia imefuzu katika fainali hiyo. Mchuano huu utatumiwa kama maandalizi muhimu kabla ya kwenda nchini Urusi.