Pata taarifa kuu
OLIMPIKI-BRAZIL 2016-RIADHA

Julius Yego amaliza wa pili katika mchezo wa urushaji mkuki

Mkenya Julius Yego ameshinda medali ya fedha katika mchezo wa kurusha mkuki katika Michezo ya Olimpiki nchini Brazil.

Julius Yego, mrusha mkuki wa Kenya aliyemaliza wa pili katika Michezo ya Olimpiki mwaka 2016 nchini Brazil
Julius Yego, mrusha mkuki wa Kenya aliyemaliza wa pili katika Michezo ya Olimpiki mwaka 2016 nchini Brazil iaaf.org
Matangazo ya kibiashara

Yego ambaye ni bingwa wa dunia, na anashikilia rekodi ya Michezo ya Jumuiya ya Madola, katika Michezo hii ya Olimpiki alirusha kwa umbali wa Mita 88.24.

Wakati wa kuelekea kwenye Michezo hii, Yego mwenye umri wa miaka 27, alikosa tiketi ya kwenda Brazil katika uwanja wa ndege jijini Nairobi na kuzua hali ya wasiwasi.

Yego aliyefahamika kwa jina la utani kama 'YouTube man' anaendelea kukumbukwa, kwa kujifunza mchezo huu wa kurusha mkuki kupitia mtandao wa Yutube na baadaye kuwa bingwa wa dunia.

Nafasi ya kwanza katika mchezo huu, ilichukuliwa na Thomas Rohler aliyerusha umbali wa Mita 90 nukta 30 na kuipa ushindi nchi yake ya Ujerumani kwa mara ya kwanza tangu Michezo ya mwaka 1972 mjini Munich.

Keshorn Walcott kutoka Trinidad & Tobago akimaliza wa tatu na kuipa nchi yake medali ya shaba kwa kurusha umbali wa Mita 85 nukta 38.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.