FFF: Karim Benzema kutoshiriki Euro 2016
Karim Benzema hatoshiriki kwa timu ya taifa ya Ufaransa katika michuano ya Kombe la mataifa ya Ulaya (Euro 2016).
Imechapishwa: Imehaririwa:
Malheureusement pour moi et pour tous ceux qui m'ont toujours soutenu et supporté. Je ne serai pas sélectionné pour notre Euro en France...
— Karim Benzema (@Benzema) April 13, 2016
Kiungo huyo wa timu ya taifa ya Ufaransa ametangaza Jumatano hii, Aprili 13, kwenye Twitter, kwamba hatochaguliwa kushiriki michuano ya Ulaya itakayopigwa nchini Ufaransa kwa kipindi cha mwezi mmoja, kuanzia Juni 10 hadi Julai 10.
Rais wa Shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF), Noël
Le communiqué @FFF sur la non sélection de @Benzema à l'@EURO2016 @RTLFrance @FFF pic.twitter.com/jGMiD5PMQV
— Jérôme MILLAGOU (@JeromeMILLAGOU) April 13, 2016
Le Graët, na kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps, wameamua kumtenga mchezaji huyo, tangazo la FFF limebainisha.
"Hata kama imetokea, Bleu siku moja ... Blue milele"
Shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF) limechukua uamuzi wake juu ya mustakabali wa mchezaji wa Real Madrid katika timu ya taifa ya Ufaransa, anayebanwa, kwa sababu ya matatizo yake ya kisheria. FFF ilitangaza "Benzegol" "hatoshirikishwa" baada ya kufanyiwa uchunguzi mwezi Novemba katika kesi ya madai ya mkanda wa usaliti kuhusu ngono dhidi ya mchezaji mwenzake wa timu ya taifa ya Ufaransa (Le Bleu) Mathieu Valbuena. Uamuzi wa Mahakama wa kumkataza kukutana na kiungo wa kati wa klabu ya Lyon, hata hivyo ulifutwa mwezi uliopita, na kupelekea shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF) kutafakari.
Quoiqu'il arrive... Bleu un jour... Bleu toujours !!!https://t.co/yHoEDzAt21
— Karim Benzema (@Benzema) April 13, 2016
Jumanne usiku, baada ya Real Madrid kufuzu nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa, Karim Benzema alisema kuwa alisubiri kwa "uaminifu" uamuzi wa FFF. Karim Benzema alirusha hewani kwenye ukurasa wake wa Facebook ujumbe uliyojaa kashfa.