FIFA-URUGUAY-UFISADI
Maafisa wa Fifa waendelea kukumbwa na kizungumkuti
Makamu wa rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA Eugenio Figueredo raia wa Uruguay amewekwa jela nchini Marekani wakati huu akisubiri kufunguliwa mashtaka kwa tuhma za ufisadi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Figueredo mwenye umri wa miaka 87 aliwekwa jela baada ya kusafirsihwa kutoka nchini Uswizi hapo jana.
Aliwahi pia kuwa rais wa Shirikisho la soka katika bara la America Kusini na miongoni mwa viongozi wa soka wa FIFA waliokamtwa jijini Zurich.
Wakili wa Figueredo anasema mteja wake huenda akapewa kifugo cha nyumbani na ikiwa atapatikana na hatia atafungwa jela miaka 15.