Pata taarifa kuu
Soka Barani Afrika-AFCON 2015

Timu ya taifa ya Tunisia yakabiliwa na vikwazo

Timu ya taifa ya Tunisia nayo huenda ikachukuliwa hatua na Shirikisho la soka barani Afrika CAF, baada ya wachezaji kumvamia refarii baada ya kukamilika kwa mchuano wa robo fainali kati yake na Equitorial Guinea.

Mchezaji wa Tunisia,Wahbi Khazri (kulia) akikabiliana na mchezaji wa Equatorial Guinea Ellong Doualla.
Mchezaji wa Tunisia,Wahbi Khazri (kulia) akikabiliana na mchezaji wa Equatorial Guinea Ellong Doualla. REUTERS/Mike Hutchings
Matangazo ya kibiashara

Katika mchuano huo, wenyeji Equatorial Guinea walipata ushindi wa mabao 2 kwa 1 na kufuzu katika hatua ya nusu fainali.

Viongozi wa CAF walikutana jana Jumatatu na kujadili suala hilo baada ya wachehaji wa Tunisia kulalamika kuwa refarii aliwapa wenyeji penalti ambayo haikustahili katika dakika za lala salama za mchuano huo.

Beki wa Equitorial Guinea Sipoto huenda naye akafungiwa na CAF kucheza katika hatua ya nusu fainali baada ya kuoneakana akimtemea mate mchezaji wa Tunisia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.