Pata taarifa kuu
BRAZIL-Kombe la dunia

Michuano ya kombe la dunia yaingia robo fainali

Michuano ya kombe la dunia inaendelea nchini Brazil, ambapo timu inne ziliyotinga robo fainali, zinajiandaa kupambana. Timu ya taifa ya Brazil inajianda kumenyana leo ijumaa na Colombia kwenye uwanja wa Fortaleza, huku Ujerumani na Ufaransa zikijiandaa kupambana kwenye uwanja wa Rio.

Kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa (les Bleus).
Kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa (les Bleus). RFI/Pierre René-Worms
Matangazo ya kibiashara

Brazil ambayo inachezea nyumbani kwa macho ya mashabiki wengi, huku Ujerumani ikiwa inavuja kwenye safu ya ushambuliaji watalazimika kuongeza nguvu katika michuano hii dhidi ya wapinzani wao.

Timu ya taifa ya Brazili (Seleção) inajiandaa kushinda mechi ya ijumaa hii dhidi ya Colombia.
Timu ya taifa ya Brazili (Seleção) inajiandaa kushinda mechi ya ijumaa hii dhidi ya Colombia. REUTERS/Paulo Whitaker

Katika mzunguko wa nane, Brazil na Ujerumani zililazimishwa kupitia kwenye kipindi cha muda wa dakika 30 za nyongeza. Vile vile Brazil ilinusurika kupitia mikwaju ya penalti (baada ya kutoka sare ya kufungana na Chili bao 1-1). katika mikwaju ya penalti, Brazil iliingiza wavuni mabao 3, huku Chili ikiingiza mabao 2.

Hayo yakijiri, Argentina-Ubelgiji na Uholanzi-Costa Rica zinajiandaa kumenyana jumamosi hii.

Rais wa Ufaransa, François Hollande.
Rais wa Ufaransa, François Hollande. REUTERS/Philippe Wojazer

 

 

 

Rais wa Ufaransa François Hollande anaandaa ijumaa hii jioni hafla ya kirafiki kati ya Ufaransa na Ujerumani kwa niaba ya mchuano huu kati ya mataifa haya mawili.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.