Serikali ya Nigeria yapanga kumlipa mshahara mnono kocha wa Super Eagles Stephen Keshi
Serikali ya Nigeria inapanga kuchukua hatua kumlipa mshahara mnono kocha wa timu ya taifa Stephen Keshi, waziri wa michezo ametangaza, na kuahidi kuwa italipa malimbikizo yote ya mishahara yake.
Imechapishwa:
Waziri wa michezo Bolaji Abdullahi amesema kuwa wamepokea kibali kutoka kwa Rais Goodluck Jonathan kuchukua madai ya mishahara ya Keshi na wasaidizi wake, ambaye anadai jumla ya Naira milioni 78 sawa na Euro 485,000,357,000
Keshi, ambaye analipwa kiasi cha naira milioni tano kwa mwezi, ingawa haijawahi kulipwa kwa takribani miezi mitano, aliiwezesha timu ya taifa ya Nigeria kushiriki michuano ya kombe la mataifa ya Africa na kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil.
Waziri wa michezo amewaambia waandishi wa habari kuwa ofisi ya rais inafanya mipango kwa ajili ya kumlipa Keshi malimbikizo ya mishahara yake yote.