Pata taarifa kuu

Vita vya Israel na Hamas: Hali ya wasiwasi yatanda kwenye mpaka wa Lebanon

Katika siku ya 95 ya vita, mkuu wa diplomasia ya Marekani yuko Tel Aviv kwa mazungumzo na viongozi wa Israeli, akitaka kusitishwa kwa mzozo kwa "lazima kabisa" ya kuwaokoa raia wa Palestina huko Gaza, iliyotumbukia katika hali mbaya ya kibinadamu. Kiongozi wa Hamas, kwa upande wake, ametoa wito kwa nchi za Kiislamu "kuunga mkono" kundi lake katika vita vyake dhidi ya Israel katika eneo hilo, kwa kuipatia "silaha". Hali ni ya wasiwasi nchini Lebanon.

Wapiganaji na wafuasi wa Hezbollah walikusanyika kwa ajili ya mazishi ya kamanda wa kijeshi wa kundi hilo, Wissam Tawil, katika mji alikozaliwa wa Khirbet Selm, kusini mwa Beirut, Jumanne hii, Januari 9, 2024.
Wapiganaji na wafuasi wa Hezbollah walikusanyika kwa ajili ya mazishi ya kamanda wa kijeshi wa kundi hilo, Wissam Tawil, katika mji alikozaliwa wa Khirbet Selm, kusini mwa Beirut, Jumanne hii, Januari 9, 2024. AFP - MAHMOUD ZAYYAT
Matangazo ya kibiashara

Unachopaswa kukumbuka:

■ Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken yuko Tel Aviv ambako ananuia kuishinikiza Israel kufanya zaidi kuwalinda raia katika Ukanda wa Gaza na kujaribu kuzuia ongezeko la mzozo wa kikanda. Aliwaambia viongozi wa Israel siku ya Jumanne kwamba kuhalalisha uhusiano na nchi za eneo hilo bado kunawezekana licha ya vita katika eneo hilo, lakini ikiwa tu Israeli itaunda mazingira ya kuunda taifa la Palestina.

■ Kiongozi wa vuguvugu la Kiislamu la Palestina Hamas, Ismaïl Haniyeh, ametoa wito kwa nchi za Kiislamu "kumuunga mkono" katika vita vyake dhidi ya Israel katika Ukanda wa Gaza kwa kumpatia "silaha".

■ Hezbollah ya Lebanon imedai kuwa imelenga kituo cha kamandi cha jeshi la Israel kaskazini mwa nchi, ili kukabiliana na kuuawa kwa naibu kiongozi wa Hamas na afisa mkuu wa kijeshi wa kundi lake.

■ Siku ya jeshi la Israel lilitangaza kwamba lilimuua "kiongozi mkuu" wa Hamas nchini Syria, aliyehusika na kurusha maroketi nchini Israeli kutoka ardhi ya Syria. Taifa la Kiyahudi kwa kawaida huwa kimya sana kuhusu operesheni zake nchini Syria, taarifa hii kwa vyombo vya habari ikiwa ni moja ya matangazo adimu katika mwelekeo huu.

■ Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu anasema "anatiwa wasiwasi sana" na "idadi kubwa" ya waandishi wa habari wa Palestina waliouawa katika Ukanda wa Gaza.

■ Kulingana na ripoti mpya iliyotangazwa Jumatatu Januari 8 na Wizara ya Afya ya Hamas, watu 23,210 wameuawa huko Gaza tangu kuanza kwa vita Oktoba 7. Wengi wa waliofariki ni wanawake, vijana na watoto. Watu karibu 60,000 walijeruhiwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.