Pata taarifa kuu

Riyadh yasitisha majadiliano juu ya uwezekano wa kurejesha uhusiano na Israeli

Saudi Arabia imeamua kusitisha majadiliano juu ya uwezekano wa kufufua uhusiano na Israeli, katikati ya vita kati ya Israel na Hamas ya Palestina, chanzo kilicho karibu na serikali ya Saudi Arabia kimeliambia shirika la habari la AFP.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken anawasili Riyadh, Saudi Arabia, Ijumaa Oktoba 13, 2023, na kulakiwa na Naibu Katibu Mkuu wa MFA wa Masuala ya Itifaki Abdulmajeed Alsmari baada ya kutua Jordan, Qatar, na Bahrain siku hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken anawasili Riyadh, Saudi Arabia, Ijumaa Oktoba 13, 2023, na kulakiwa na Naibu Katibu Mkuu wa MFA wa Masuala ya Itifaki Abdulmajeed Alsmari baada ya kutua Jordan, Qatar, na Bahrain siku hiyo. AP - Jacquelyn Martin
Matangazo ya kibiashara

Saudi Arabia "imeamua kusitisha majadiliano juu ya uwezekano wa kufufua uhusiano na Israel na imewajulisha maafisa wa Marekani," amesema, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken, ambaye amezuru Riyadh katika sehemu ya ziara ya kikanda.

Zaidi ya majengo 1,300 yaharibiwa huko Gaza

Zaidi ya majengo 1,300 yameharibiwa kabisa katika Ukanda wa Gaza, Umoja wa Mataifa umesema, baada ya wiki moja ya mashambulizi makali ya wanajeshi wa Israel.

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema nyumba 5,540 "ziliharibiwa", wakati karibu zingine 3,750 ziliharibiwa kabisa na haziwezi kukaliwa na watu.

“Tunashuhudia mauaji makubwa na ya kimakusudi ya raia katika eneo hili,” asema Jean-François Corty, naibu mkuu wa shirika la Médecins du Monde kuhusu hali huko Gaza.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.