Pata taarifa kuu

Mageuzi ya mfumo wa mahakama Israel: Wiki ya maamuzi huanza

Mjadala juu ya mageuzi ya mfumo wa mahakama unazinduliwa upya. Mnamo Jumanne, Septemba 12, Mahakama ya Juu itachunguza mojawapo ya vipengele muhimu vya mradi huo, sheria ambayo inadhoofisha udhibiti wa idara ya mahakama dhidi ya serikali na Bunge (Knesset).

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akila kipande cha tufaha kuadhimisha Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Kiyahudi, wakati wa mkutano wake wa kila wiki wa baraza la mawaziri mjini Jerusalem, Jumapili hii, Septemba 10, 2023.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akila kipande cha tufaha kuadhimisha Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Kiyahudi, wakati wa mkutano wake wa kila wiki wa baraza la mawaziri mjini Jerusalem, Jumapili hii, Septemba 10, 2023. AP - Ohad Zwigenberg
Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Israel, Michel Paul

Kwa wengi, hii ni wiki ya maamuzi ambayo inafunguliwa. Kuanzia Jumatatu asubuhi, maandamano ya kupinga mageuzi ya mfumo wa mahakama yanapangwa kufanyika.

Lakini alasiri kutakuwa na mkusanyiko mkubwa mbele ya Mahakama ya Juu ya Israeli huko Jerusalem. Siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita, mrengo wa kulia nchini Israeli ulifanya mkutano mkubwa wa kuunga mkono mradi wa kurekebisha mfumo wa mahakama.

Kesho Jumanne, majaji kumi na watano wa Mahakama Kuu watakutana ili kuamua hatima ya sheria inayofuta kile kinachoitwa kifungu cha "busara". Kamwe sheria ya aina hii haijawahi kufutwa na majaji wa Mahakama ya Juu. Ni mawaziri watatu tu kati ya 32 katika serikali ya Benjamin Netanyahu ambao wametangaza wazi nia yao ya kukubali uamuzi wowote wa chombo cha juu zaidi cha mahakama.

Mgogoro wa kikatiba unaonekana kutoepukika. Isipokuwa, kama wachambuzi kadhaa wanavyodai, Benjamin Netanyahu ataamua mwenyewe katika dakika ya mwisho kupendekeza sheria mpya, katika toleo lisilopuuzwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.