Pata taarifa kuu

Iran: Watu watano wahukumiwa kifo kwa mauaji ya mwanamgambo wa Kiislamu

Mahakama ya Iran imetangaza hukumu mpya za kifo dhidi ya watu watano huku kukiwa na miito ya mgomo wa siku tatu na maandamano kuanzia Jumatatu tarehe 5 hadi siku ya Jumatano.

Picha iliyopigwa Novemba 24, 2022 inaonyesha picha za wahanga wa utawala wa Iran wakiwa wameweka sakafuni huku waandamanaji wakipeperusha bendera za Iran kabla mapinduzi ya Kiislamu nje ya makao makuu ya Umoja wa Mataifa wakati wa kikao maalum cha Baraza la Haki za Binadamu kuhusu hali nchiniIran, huko Geneva.
Picha iliyopigwa Novemba 24, 2022 inaonyesha picha za wahanga wa utawala wa Iran wakiwa wameweka sakafuni huku waandamanaji wakipeperusha bendera za Iran kabla mapinduzi ya Kiislamu nje ya makao makuu ya Umoja wa Mataifa wakati wa kikao maalum cha Baraza la Haki za Binadamu kuhusu hali nchiniIran, huko Geneva. © AFP - VALENTIN FLAURAUD
Matangazo ya kibiashara

Jumla ya watu kumi na watano wamehukumiwa kwa mauaji ya mwanamgambo wa Kiislamu au bassidji wiki chache zilizopita. Watu watano walihukumiwa kifo na wengine hukumu nzito.

Video ya mauaji hayo ilisambaa sana kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya serikali na ilitumika katika kesi hiyo. Katika video hiyo kunaonekana watu wapatao thelathini wakimshambulia kijana kwa kisu na mawe, pia wakimpiga teke.

Hukumu mpya za kifo zilitangazwa huku waandamanaji wanne au wasumbufu, kulingana na mamlaka, walinyongwa Jumapili asubuhi.

Kadhalika, mkuu wa mahakama alitangaza kunyongwa katika siku zijazo kwa watu waliopatikana na hatia ya mauaji wakati wa maandamano ya wiki chache zilizopita.

Jumanne hii, kulikuwa na maduka machache yaliyofungwa katika mji mkuu kuliko Jumatatu. Jana usiku, makundi madogo ya vijana walifanya maandamano katika vitongoji kadhaa vya Tehran, huku wakizuia njia na barabara kuu katika mji mkuu.

Wakati huo huo, msemaji wa vyombo vya sheria ametangaza kwamba waandamanaji 1,200 waliokamatwa katika wiki za hivi karibuni wameachiliwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.