Pata taarifa kuu
YEMEN-USALAMA

Usitishwaji mapigano kwa miezi miwili nchini Yemen: Ufaransa yakaribisha 'hatua muhimu'

Ufaransa imekaribisha "muhimu" wakati nchini Yemen, makubaliano ya usitishwaji vita kwa kipindi cha miezi miwili yaliyofikiwa kati ya serikali na waasi wa Houthi yanatarajiwa kuanza kutekelezwa Jumamosi hii, Machi 2 mchana, chini ya mwavuli wa Umoja wa Mataifa. Waasi wa Houthi wako katika vita nchini Yemen kwa kipindi cha miaka minane.

Yemen inaendelea kusakamwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.
Yemen inaendelea kusakamwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe. AP - Nariman El-Mofty
Matangazo ya kibiashara

Siku ya Ijumaa Umoja wa Mataifa ulitangaza kwamba pande zinazokinzana nchini Yemen zimefikia makubaliano ya usitishwaji mapigano kwa kipindi cha miezi miwili.

"Wapiganaji wameitikia vyema pendekezo la Umoja wa Mataifa la kusitishwa mapigano kwa kipindi cha miezi miwili ambacho kitaanza kutekelezwa kesho saa moja usiku jioni," mjumbe wa Umoja wa Mataifa kwa Yemen Hans Grundberg amesema katika taarifa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.