Marekani yaendelea na mazungumzo na Taliban Doha
Wajumbe wa Marekani wanaendelea na mazunguzo na wawakilishi wa kamati ya kisiasa ya Taliban iliyoko Doha nchini Qatar, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imebaini, baada ya Taliban kuuteka mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.
Imechapishwa:
Pamoja na kukimbia kwa rais wa Afghanistan Ashraf Ghani kando na kuwasili kwa Taliban katika mji mkuu, mazungumzo sasa yanalenga kuzuia vurugu badala ya kujadili makubaliano ya amani, kama ilivyokuwa, Aamesema msemaji wa Wizara ay mambo ya Nje ya Marekani.
Alipoulizwa ni serikali gani ambayo Marekani itaunga mkono kama halali nchini Afghanistan, Ned Price amesema Washington inashauriana na jamii ya kimataifa, akibainisha kuwa hakuna makabidhiano rasmi yaliyofanyika jijini Kabul.