Pata taarifa kuu
AFGHANISTAN-USALAMA

Mapigano Afghanistan : Kabul na Washington walaumiana kufautia

Vita vya maneneo vyaibuka kati ya Marekani na Afghanistan baada ya Taliban kuyateka maeneo kadhaa ya Afghanistan, huku kila upande ukilaumu wengine, wakati vita vinaendelea.

Mwanajeshi wa Jeshi la Afghanistan akitoa ulinzi kando ya barabara wakati wa mapigano yanayoendelea kati ya Talian na vikosi vya usalama vya Afghanistan katika mkoa wa Herat, Agosti 1, 2021.
Mwanajeshi wa Jeshi la Afghanistan akitoa ulinzi kando ya barabara wakati wa mapigano yanayoendelea kati ya Talian na vikosi vya usalama vya Afghanistan katika mkoa wa Herat, Agosti 1, 2021. AFP - HOSHANG HASHIMI
Matangazo ya kibiashara

Marekani inasema inasikitishwa na hatua ya maafisa wa usalama nchini Afghanistan kushindwa kuzuia kundi la Taliban kuendelea kuchukua udhibiti wa miji kadhaa, licha ya kutumia Mabilioni ya Dola kuwapa mafunzo na silaha kwa miaka 20.

Serikali ya Afganistan inailaumlu Marekani kwa kuondoa majeshi yake kama sababu ya kuzorota kwa hali ya usalama nchini humo, wakati huu ikipanga kuyapa silaha makundi ya wapiganaji kusaidia kupambana na Taliban.

Wapiganaji wa Taliban wamekamata zaidi ya robo ya miji mikuu ya mikoa ya nchi hiyo katika kipindi cha chini ya wiki moja.

Wakati huo huo mjumbe maalum wa Marekani kwa Afghanistan Zalmay Khalilzad yuko Doha ambako anajaribu kuwashinikiza viongozi wa Taliban kukubali mpango wa usitishwaji wa mapigano.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.