Taarifa za kupotosha kuwa jeshi limefanya mapinduzi Congo-Brazzaville
Imechapishwa:
Cheza - 09:59
Wiki mbili zilizopita mitandao ya kijamii ilijaa chapisho kuhusu habari za kupotosha kuhusu mapinduzi ya kijeshi nchini Congo Brazaville
Lakini Serikali ilikanusha ripoti hizi. Kwenye mtandao wa X zamani ukiitwa Twitter, msemaji wa serikali Thierry Moungala alichapisha ujumbe akisema
“Tunawahakikishia watu kuwa hakuna vurugu na tunawashauri warudi na kuendelea na shughuli zao leo na kesho.”
Chapisho lingine likiwa na hashtag, habari za hivi punde, lilisema hivi
“Jeshi la Kongo limepindua serikali ya rais Denis Sassous Nguesso ambaye alikuwa jijini NewYork. Jeshi limechukua udhibiti wa majengo muhimu katika jiji la Brazzaville. Chapisho liliendelea kusema kuwa kwa mujibu wa ripoti za awali, mwanzilishi wa mapinduzi ni kamanda fulani wa walinzi wa rais.