Mazishi ya Moi: Viongozi kutoka Afrika Mashariki wahudhuria ibada ya kitaifa
Marais mbalimbali kutoka eneo la Afrika Mashariki wameungana na Wakenya, katika ibada ya kitaifa ya kumuaga aliyekuwa rais wa nchi hiyo Daniel Toroitich Arap Moi, aliyefariki dunia wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 95.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Waombolezaji waliwasili mapema katika uwanja wa taifa wa Nyayo jijini Nairobi kuhudhuria ibada hiyo, katika uwanja huo ulionjegwa na rais huyo wa zamani waKenya.
We should learn from Moi's inspiring journey and the chronicles of his life. He will be laid to rest but will continue to live on in every one of us. President Uhuru Kenyatta #MoiFinalJourney pic.twitter.com/t3cn3SdetI
NTV Kenya (@ntvkenya) February 11, 2020
Jeshi la Kenya, lilihusika pakubwa katika maombolezo hayo, huku bendi ikicheza nyimbo za huzuni.
Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta, amemkumbuka rais huyo wa zamani kama mtu aliyependa upendo na amani.
Aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga alisema kwamba japokuwa mzee Moi alikuwa na makosa alisaidia katika kutengeneza katiba mpya mbali na kuleta elimu kwa wote pamoja na maziwa ya nyayo. Raila alisema kwamba mzee Moi anafaa kukumbukwa kwa mazuri aliyotenda badala ya mabaya anayohusishwa nayo.
Viongozi mbalimbali kutoka mataifa ya Afrika Mashariki nao pia walipata fursa ya kumkubuka Moi, rais Magufuli ambaye hotuba yake ilisomwa na rais mstaafu Benjamin Mkapa akiandamana na mrithi wake Jakaya Mrisho Kikwete alisema kwamba uhusiano mzuri kati ya Kenya na Tanzania umeendelea kuwepo kutokana na uongozi wa rais Moi.
Former Tanzania's President Benjamin Mkapa pays his tribute to Mzee Moi and reads President John Magufuli's tributes at Nyayo Stadium. #RIPMoi pic.twitter.com/D71TbH4RbJ
K24 TV (@K24Tv) February 11, 2020
Mkapa alisema kwamba licha ya kufanya kazi na Moi alimtaja pia kama mshauri wake mkuu.
Naye rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kwamba rais mstaafu atakumbukwa kwa mazuri aliyoleta nchini Kenya na eneo la Afrika mashariki kwa ujumla. Alisema kwamba Moi alikuwa dawa ya kenya kwa kuwa aliweza kuliongoza taifa hili bila ya migogoro.
Museveni says Kenyans are lucky to have leaders like Moi
Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) February 11, 2020
https://t.co/NQSraNiIkI
Alisema kwamba hatua yake ya kukiongoza chama cha KADU kufanya muungano na KANU ilikuwa dhihirisho tosha kwamba ni kiongozi aliyetaka mshikamano wa nchi.
Rais wa Rwanda Paul Kagame walimsifu mzee kama kiongozi aliyeunganisha makabila tofauti nchini Kenya na kuleta amani katika eneo zima la Afrika mashariki.
Moi atazikwa kesho nyumbani kwake huko Kabarak katika kaunti ya Nakuru na atakumbukwa kuongoza taifa hilo kwa miaka 24, na licha ya kusifiwa kwa kuleta umoja wa kitaifa nchini Kenya, waliomfahamu zaidi wanakiri kuwa, alifanya makosa mbalimbali kama binadamu.