Pata taarifa kuu
BURUNDI-ICC-HAKI

ICC yaruhusu kufanyika kwa uchunguzi kuhusu uhalifu uliofanywa Burundi

Majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita ya ICC wameidhinisha rasmi kufanyika kwa uchunguzi wa kina kuhusu tuhuma za kutekelezwa kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu nchini Burundi, ambako zaidi ya watu elfu 1 na 200 wamekufa tangu kulipozuka machafuko mwaka 2015.

Maiti ya mtu asiejulikana katika moja ya mitaa ya mji wa Bujumbura, Desemba 12, 2015.
Maiti ya mtu asiejulikana katika moja ya mitaa ya mji wa Bujumbura, Desemba 12, 2015. REUTERS/Jean Pierre Aime Harerimana
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa maofisa wa mahakama hiyo, wamesema kuwa uamuzi wa majaji ulifanyika mwezi uliopita, siku mbili tu kabla ya Octoba 27 mwaka huu nchi Burundi kuwa taifa la kwanza kujitoa kwenye mahakama hiyo.

Kwenye uamuzi wao, majaji wamemruhusu mwendesha mashtaka mkuu Fatou Bensouda kuanzisha uchunguzi kuhusu makosa yaliyofanyika nchini Burundi au kufanywa na raia wake wanaoishi nje ya nchi kuanzia April 26 mwaka 2015 hadi Octoba 26 mwaka 2017.

Fatou Bensouda anaweza kupanua wigo wa uchunguzi wake kwa makosa yaliyotekelezwa kabla na baada ya tarehe hizo ikiwa misingi kadhaa ya kisheria itafikiwa.

Tayari msemaji wa rais Pierre Nkurunziza Willy Nyamitwe kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter amekashifu uamuzi huu wa majaji aliosema ni sawa na kujipiga risasi mguuni.

Mahakama hiyo inasema licha ya kuwa Burundi imejitoa rasmi Octoba 27, majaji wamesisitiza kuwa wanayomamlaka ya kuafanya uchunguzi kuanzia tarehe zilizotajwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.