KENYA-AJALI
Ajali yasababisha vifo vya watu 11 Pwani ya Kenya
Watu 11 wamepoteza maisha katika ajali ya barabara katika Kaunti ya Tana River Pwani ya Kenya.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kamanda wa Polisi katika Kaunti hiyo Walter Aliwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo katika barabara kuu ya Bangal.
Ripoti zinasema kuwa ajali hiyo ilitokea saa tisa alfajiri wakati basi hilo likielekea jijini Nairobi, kutoka Wajir.
Abiria nane walikuwa ndani ya basi hilo huku wengine watatu wakiwa ndani ya Lori, lililogongana ana kwa ana na basi hilo la abiria.
Walioponea ajali hiyo wanasema basi hilo liikuwa linaendeshwa kwa mwendo wa kasi.