Siku ya Kimataifa ya wanawake 2024: Plan International Kenya inavyowafikia wanawake nchini Kenya
Kila tarehe 8, Machi kila mwaka, dunia huadhimisha siku ya Kimataifa ya wanawake.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Cheza - 03:35
Kauli mbinu ya mwaka 2024 ni kuwekeza kwa wanawake, kufanikisha maendeleo yao.
Nchini Kenya, kama ilivyo kwenye nchi zingine za Afrika, ongezeko la mizozo inayohusishwa na vita, madhara hasi ya mabadiliko ya tabia nchi, waathiriwa wengi ni wanawake na watoto.
Shirika la Plan International Kenya, limekuwa likiwafikia wanawake wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali kama njaa na mahitaji muhimu kwa wasichana kama taulo za hedhi.
Mwandidhi wetu wa masuala ya afya, Carol Korir, amezungumza na Annah Katuki afisa wa jinsia katika Shirika hilo.