Pata taarifa kuu

Bernard Membe, Waziri wa zamani wa Mambo ya nje wa Tanzania afariki dunia

NAIROBI – Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Bernard Membe amefariki dunia, jijini Dar es salaam. 

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Bernard Membe
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Bernard Membe © bernard Membe
Matangazo ya kibiashara

Rais Samia Suluhu Hassan, amesema amepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha Membe, ambaye pia aliwahi kuwania urais mwaka 2020, kupitia chama cha ACT Wazalendo. 

“Kwa zaidi ya miaka 40, Ndugu Membe alikuwa mtumishi mahiri wa umma, mwanadiplomasia, Mbunge na Waziri aliyeitumikia nchi yetu kwa weledi,” ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter. 

Ripoti kutoka kwa aliyekuwa Msaidizi wake, Allan Kiluvya zimesema, Membe aliugua kwa muda mfupi na kukimbizwa hospitalini, Ijumaa Alfajiri  na baadaye akafariki. 

Alihudumu katika nafasi ya Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa kati ya mwaka  2007 hadi 2015, wakati wa uongozi wa rais mstaafu Jakaya Kikwete. 

Membe aliwahi pia kuwa Mbunge wa jimbo la Mtama, alikochaguliwa mwaka 2000 na kuhudumu hadi mwaka 2015. 

Shirika la habari linalomilikiwa na serikali nchini humo pia limethibitisha kifo cha Membe.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.