Pata taarifa kuu
EAC

Viongozi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakutana kujadili usalama Mashariki mwa DRC

Marais wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, wamekutana jijini Bujumbura nchini Burundi katika mkutano usiokuwa wa kawaida, kujadiliana kuhusu kuendelea kwa mzozo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Viongozi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakikutana jijini Bujumbura, Februari 4 2023 kwenye mkutano usiokuwa wa kawaida kujadili hali ya usalama, Mashariki mwa DRC
Viongozi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakikutana jijini Bujumbura, Februari 4 2023 kwenye mkutano usiokuwa wa kawaida kujadili hali ya usalama, Mashariki mwa DRC © jumuiya
Matangazo ya kibiashara

Viongozi hao wamekutana kutathmini mwenendo wa hali ya usalama, Mashariki mwa DRC na nini cha kufanya kurejesha amani, katika kipindi hiki ambacho waasi wa M23 wanapoendelea kupambana na vikosi vya DRC na kuchukua maeneo zaidi.

Rais wa DRC Felix Thisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame, ambao nchi zao hazina uhusiano mzuri wa kidiploamsia kuhusu madai ya kuwaunga mkono waasi wa M23 pia wamehudhuria.

Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Yoweri Museveni wa Uganda, Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, William Ruto wa Kenya na mwakilishi wa Sudan Kusini.

Rais Felix Tshisekedi (DRC), William Ruto (Kenya)  na Yoweri Museveni (Uganda) miongoni mwa viongozi waliohudhuria mkutano wa viongozi wa Jumuiya jijini Bujumbura, Februari 4 2023
Rais Felix Tshisekedi (DRC), William Ruto (Kenya) na Yoweri Museveni (Uganda) miongoni mwa viongozi waliohudhuria mkutano wa viongozi wa Jumuiya jijini Bujumbura, Februari 4 2023 © jumuiya

Mkutano huu umekuja siku chache baada ya Rwanda kukiri kushambulia ndege ya kivita ya DRC, baada ya kudai kuwa ilivuka mpaka na kuingia kwenye angaa lake kinyume cha sheria.

DRC nayo imewafukuza wanajeshi wa Rwanda, waliokuwa katika ujumbe wa jeshi la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hizi ni baadhi ya changamoto zinazosubiri viongozi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kuyatafutia ufumbuzi.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.