Pata taarifa kuu
SUDAN KUSINI

Kundi jipya lateka Mayom Kaskazini mwa jiji la Juba

Nchini Sudan Kusini, kundi  jipya la waasi limedhibiti Kaunti ya Mayom, Kaskazini mwa jiji kuu Juba, na kuzua hali ya wasiwasi, wakati huu nchi hiyo inapoendelea kukabiliwa na utovu wa usalama, tangu kutiwa saini kwa mkataba wa amani mwaka 2018.

Wanajeshi wa Sudan Kusini
Wanajeshi wa Sudan Kusini REUTERS/George Philipas
Matangazo ya kibiashara

Kundi hilo ambalo linajiita  People’s Army of  South Sudan,  linaongozwa na mwanajeshi aliyeasi katika jeshi  la Sudan Kusini: Meja-Jenerali Steven Buoy Roinyang.

Niko kwenye uwanja wa mapigano hapa mayom. Tumeanzisha kundi jipya linalotambulikana kama South Sudan People’s Army, kwa njia nyingine South Sudan People’s Army. Tunalenga kuiangusha serikali iliyoko sasa ili tuwape wananchi wa Sudan kusini  fursa ya kuwachagua viongozi wao katika uchaguzi huru na wa haki.

Waziri Wa Habari, Michael  Makwei, alikataa kuzungumzia suala hilo na kumwachia Mkuu wa Majeshi aliyekuwa na kauli hii.

Wanajeshi wetu wameanzisha msako mkubwa ukiwa na madhumuni ya kumnasa kiongozi wa waasi. Hatua kali itachukuliwa. Atalipa gharama kubwa kutokana na uasi aliotekeleza.

Sudan Kusini ina makundi kumi ya waasi. Makundi manane yalisaini mkataba wa amani ambao  ulileta serikali inayotawala sasa. Wanajeshi waasi tiifu kwa Meja-Jenerali Steven Buoy Roinyang, wanadhihirisha jinsi hali ilivyo ngumu ya kuimarisha amani nchini Sudan Kusini, miaka kumi-na-moja baada ya kutangazwa kama nchi huru.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.