Tume ya Uchaguzi yasikiliza rufaa za wanasiasa waliokataliwa kuelekea Uchaguzi Mkuu
Nchini Kenya, Tume ya Uchaguzi inasikiliza rufaa za baadhi ya wanasiasa waliokataliwa, kwa kutofikia vigezo vya kuwania urais, kuelekea uchaguzi wa mwezi wa nane.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Miongoni mwa wanasiasa hao ni Wakili Ekuru Aukot kutoka chama cha Thirdway Alliance, hapa anaeleza ni kwanini alikata rufaa kwa Tume ya Uchaguzi.
Ekuru Aukot
“ Chebukati hakufuata sheria na sisi tutampeleka mahakamani tumkumbushe sheria.” amesema Aukot.
Mfanyabiashara Jimi Wanjigi, aliyekuwa na matumaini ya kuwania urais, kupitia chama cha Safina, naye alikataliwa, anaamini alizuiwa kwa sababu za kisiasa.
Make no mistake, we are living in the age of Oppression. We Must & we will stand up to those who wish to soil and tarnish our hard gained democracy. #Itwika #WeAreFearless #JimiWillis pic.twitter.com/1uGbmIJIx6
— Jimi Wanjigi (@JimiWanjigi) June 9, 2022
Jimmy Wanjigi
“Huu ni utapeli, ni kana kwamba kuna Mwenyekiti mwingine wa Tume ya Uchaguzi," ameongezea Wanjigi.
Wiki moja, iliyopita, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Wafula Chebukati, alitangaza majina ya wagombea wanne, waliokidhi vigezo vya kikatiba kuwania urais, na hao ni pamoja na Naibu rais William Ruto, Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga na Mawakili Profesa Goerge Wajakoya na Wahiga Mwaure.
IEBC Chairman Wafula Chebukati presides over the launch of the Commission Dispute Resolution Committee Hearings at the Milimani Law Courts #GE2022 pic.twitter.com/xx6o60354W
— IEBC (@IEBCKenya) June 11, 2022
Rufaa hizo zinatarajiwa kumalizika mwishoni mwa wiki hii, kuamua hatima ya watu 160 waliokataliwa na Tume ya Uchaguzi kuwania nyadhifa mbalimbali.