Pata taarifa kuu
Rwanda - Jamii

Rwanda : Mahakama yamuondolea Dieudonné Ishimwe mashtaka ya ubakaji

Mahakama ya Kigali imefuta kesi ya ubakaji dhidi ya mwandalizi wa mashindano ya Miss Rwanda, Dieudonné Ishimwe, ila mahakama hiyo imesema Ishimwe atashtakiwa kwa makossa mengine yanayohusiana na unyanyasaji wa kingono.

Mkurugezi mkuu wa mashindano ya Miss Rwanda,
Dieudonné Ishimwe.
Mkurugezi mkuu wa mashindano ya Miss Rwanda, Dieudonné Ishimwe. © miss Rwanda
Matangazo ya kibiashara

Mahakama hiyo pia imemunyima Ishimwe dhamana baada ya kumatwa kwake mwezi uliopita, akihusishwa na madai ya kuwanyanyasa kingono wasichana wanaoshiriki mashindano ya Miss Rwanda, mashtaka ambayo ameyakanusha.

Mahakama imesema hakuna ushahidi wa kutosha kumfungulia Ishamwe mashtaka ya ubakaji, ila anaweza kufunguliwa mashtaka ya unyanyasaji wa kingono.

Shuktama dhidi ya Ishimwe ni miongoni mwa mijadala ambayo inagonga vichwa vya habari nchini Rwanda, baadhi ya raia wakihusisha mashataka hayo na siasa, serikali  nayo ikilazimika kufuta mashindano ya mwaka huu ya Miss Rwanda kutokana na shutama hizo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.