Kenya: Joto la kisiasa laendelea kutokota kuelekea uchaguzi
Nchini Kenya, naibu rais William Ruto anayeongoza muungano wa Kenya Kwanza, amesaini mkataba wa ushirikiano kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Ruto atakayewania urais kupitia muungano huo unaoundwa na zaidi ya vyama 10, amesema muungano huo utaleta mabadiliko nchini Kenya ukiingia madarakani.
Katika hatua nyingine, muungano wa Azimio One Kenya, ambao mgombea wake ni kiongozi wa muda mrefu wa upinzani Raila Odinga, umekanusha madai kuwa kuna mpasuko kati ya vyama mbalimbali.
Kazi kubwa iko mbele ya miungano hiyo miwili ni kumtafuta wagombe wenza kuelekea kuanza kwa kampeni rasmi mwezi ujao.