Samia Suluhu azuru Rwanda na kutia saini mikataba mbalimbali na mwenyeji wake
Rais wa Tanzania ,Samia Suluhu Hassan yupo nchini Rwanda ziara ya siku mbili ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuingia madarakani mwezi Mei.
Imechapishwa:
Baada ya kuwasili jijini Kigali, viongozi hao wawili wamejadiliana na kutiliana saini kuhusu ushirikiano wa masuala ya kiuchumi na teknolojia yanayolenga kuimarisha mahusiano kati ya mataifa hayo mawili.
Naye rais Kagame amesema, ni muhimu kwa mataifa hayo mawili na mengine kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki kuendeleza ushirikiano hasa dhidi ya kushinda janga la Covid 19.
Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni alizuru Kenya, Uganda na Burundi na sasa ana zuru Rwanda kwa lengo la kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo na Tanzania.