Marekani kushirikiana na Tanzania kupambana na Covid 19
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan siku ya Jumanne alifanya mazungumzo na Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Antony Blinken.
Imechapishwa:
Mazungumzo hayo yaliyojikita zaidi kwenye ushirikiano wa nchi hizo mbili kupambana na maambukizi ya Covid-19.
Wiki iliyopita, rais Samia alidokeza kuwa nchi hiyo ina wagonjwa wa corona katika wimbi la tatu la maambukizi hayo na kutoa wito kwa wananchi wa taifa hiyo kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga.
Katika mtandao wake wa Twitter, Blinken amesifu jitihada za kiongozi huyo wa Tanzania kwa kufungua ukurasa mpya katika makabiliano ya janga la Corona.
I had a productive conversation with Tanzanian President Hassan today. Our partnership is strong and enduring, and together we are working to ensure a peaceful, prosperous future for all Tanzanians – this includes our continued cooperation to fight the COVID-19 pandemic.
— Secretary Antony Blinken (@SecBlinken) July 6, 2021
Marekani imeahidi, kuisadia Tanzania katika mapambano hayo. Mazungumzo hayo pia yaligusia kuhusu namna ya kuimarisha demokrasia kwa kuheshimu haki za kisiasa, za mashirika ya kiraia na uhuru wa vyombo vya Habari.
Aidha, viongozi hao wawili wamejadiliana kuhusu masuala ya usalama na mchango wa Tanzania kutuma wanajeshi wa kulinda amani hasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.