SADC kupeleka wanajeshi wa jumuiya hiyo maeneo ya mipaka kati ya Msumbiji na Tanzania
Mataifa ya Jumuiya ya Kusini mwa Afrika SADC, yamekubaliana kutuma wanajeshi nchini Msumbiji kukabiliana na wanajihadi katika mkoa wa Cabo Delgado ambao unashuhudia changamoto za kiusalama, Kaskazini mwa nchi hiyo.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Hata hivyo, haijafahamika kwa kina kuhusu kikosi hicho na muda ambao kitatumia kukabiliana na manajihadi hao, lakini mapema mwaka huu, iliropotiwa kuwa SADC inatarajiwa kutuma wanajeshi 3,000 nchini humo.
Mwenyeji wa mkutano huo, rais Filipe Nyusi wa Msumbiji ambaye pia ni mwenye kiti wa sasa wa Jumuiya ya SADC aliitisha mkutano huo ili kuomba usaidizi wa marais wenzake kuhusu kitisho cha wanamgambo wanaohusishwa na kundi linalojiita Islamic State IS, ambao wamekuwa wakiendesha mashambulizi katika jimbo la Capo Delgado,kaskazini mwa Msumbiji
Katibu mtendaji wa jumuiya ya SADC, Stragomena Pax amesema marais hao wamekubaliana kupeleka kikosi cha pamoja cha jumuiya hiyo nchini Msumbiji ili kuimarisha usalama wa eneo hilo, huku wakitoa wito wa kupewa msaada wa kimataifa katika mapambano yake dhidi ya ugaidi.
Wapiaganaji wa kigaidi wameshutumiwa kwa kufanya mauaji ya kikatili tangu mwaka 2017 kwa kufanya uvamizi wa vijiji na miji maeneo ya mpaka kati ya Msumbiji na Tanzania.