SUDAN - UCHUMI
IMF yaidhinisha mkopo wa dolla billioni 2.5 kwa Sudan
Shirika la Fedha la duniani IMF, limeidhinisha mkopo wa dolla billioni 2.5 kwa taifa la Sudan.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
IMF imetoa tangazo hilo wakati huu ikimalizia makubaliano na mataifa fadhili 101 ya sudan , kuruhusu Sudan kulipa dini lake la dolla billioni 1.4, kutoka kwa wakopeshaji wa Marekani, ili Sudan iruhusiwe kupata mikopo zaidi.
Haya yanajiri wakati huu maandamano yakitarajiwa katika jiji la Khartoum, nchini Sudan, wandamanaji wakilalamikia mageuzi mapya serikali katika sekta ya uchumi.
Wandamanaji wanadai kuwa mfumo mpya wa uchumi nchini humo umechangia maisha kuwa magumu wakitaka serikali kuweka mikakati kuwasaidia raia wa kawaida.