Pata taarifa kuu
KENYA-QATAR-HAKI

Qatar: Mkenya Malcolm Bidali azuiliwa kwa wiki tatu bila mashtaka yoyote

Malcolm Bidali, raia wa Kenya, amezuiliwa nchini Qatar kwa wiki tatu na mashtaka dhidi yake bado hayajulikani. Mlinzi huyo amekuwa akiandika, kwa jina bandia, juu ya hatima ya wafanyakazi wahamiaji nchini humo.

Wafanyakazi katika mtaa moja huko Doha, mji mkuu wa Qatar, Machi 17, 2020.
Wafanyakazi katika mtaa moja huko Doha, mji mkuu wa Qatar, Machi 17, 2020. AFP - KARIM JAAFAR
Matangazo ya kibiashara

"Anazuiliwa kwa usiku wa ishirini bila mashitaka yoyote". Kwenye ukurasa wake wa twitter, Vani Saraswathi amekuwa akihesabu idadi ya siku tangu Malcolm Bidali akamatwe. Ni mhariri mkuu na mkurugenzi wa mradi wa Migrant-Rights, shirika la haki za wahamiaji lililoko katika nchi za Ghuba. Ni kwenye wavuti huo Mkenya huyo aliandika kwa jina bandia la "Noah".

Katika kilele cha tukio  hilo, Malcolm Bidali alifafanua maisha yake ya kila siku kama mlinzi huko Qatar. Ushuhuda adimu, ulioandikwa kwa mtu wa kwanza, ambaye anaweza kuwa chanzo cha kukamatwa kwake, mashirika makubwa yanayotetea haki za binadamu yamesema.

Kwa kweli, sababu hasa ya kukamatwa kwake bado haijulikani. Kijana huyo wa miaka 28 "anachunguzwa kwa kukiuka sheria na kanuni za usalama," mamlaka ya Qatar imesema.

Wakati Kombe la soka la Dunia la mwaka 2022 linakaribia, mambo ya Bidali bado ni mwiba mwingine kwa Qatar. Kwa miezi kadhaa, kampeni ya kususia michano hiyo ya kimataifa imeshutumu jinsi wafanyakazi wahamiaji wanavyofanyiwa madhila nchini humo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.