Burma yatengwa kwenye mkutano wa ASEAN
Nchi jirani kwa na Burma zinakusudia kuidhinisha vikwazo dhidi ya viongozi wa kijeshi wa Burma ambao hawaheshimu ahadi za kisiasa zilizotolewa Jumuiya ya kikanda ya nchi za Kusini Mashariki mwa Asia, ASEA, za kurejesha amani nchini Burma.
Imechapishwa:
Wakati wa mkutano uliodumu kwa zaidi ya saa mbili, siku ya Ijumaa, Oktoba 15, mawaziri wa mambo ya nje wa nchi kumi za ukanda wa Asean (Jumuiya ya kikanda ya nchi za Kusini Mashariki mwa Asia) waliamua kwamba kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Burma Min Aung Hlaing hatashiriki mkutano wa kilele unaokuja wa kundi hilo. Mkutano huo umepangw Kwa swali, mtazamo wa majenerali ambao hawaheshimu ahadi zao: wanakataa katu katu mapendekezo ya mjumbe maalum wa ASEAN, Erywan Yusof, Naibu Waziri wa Mambo ya nje wa Brunei, aliyeteua mjumbe wa wa ASEAN kwa Burma baada ya miezi kadhaa ya mazungumzo. Aliomba hasa kuweza kukutana na kiongozi wa zamani wa Burma Aung San Suu Kyi, ambaye alipinduliwa mamlakani mwezi Februari na ambaye bado yuko kizuizini. Kwa kweli, ziara ya mjumbe huyu maalum inaahirishwa kila mara na hali ya vita kwenye uwanja wa mapambano inazidi kuwa mbaya. Taarifa hiyo ilisema "maendeleo hayatoshi" katika utekelezaji wa mpango wa masuala matano, uliopitishwa mwezi Aprili, ambao ungelisaidia kuanzishwa kwa mazungumzo nchini Burma na kuwezesha kuwasili kwa misaada ya kibinadamu.Majenerali hawaheshimu ahadi zao
Mstari mgumu