Korea Kusini: Mafuriko yaua 13, maelfu watoroka makazi yao
Watu 13 wamepoteza maisha kufuatia kisa cha mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha nchini Korea Kusini katika siku za hivi karibuni na kusababisha maelfu ya watu kutoroka makazi yao.
Imechapishwa:
Watu wengine kumi na tatu hawajulikani waliko kulinga na na vyanzo kutoka idara ya taifa ya kupambana na majanga.
Wawakilishi wa kikosi cha Zimamoto na Uokoaji wamesema kuwa maji yameharibu zaidi ya hekta 5,751 za mashamba na kusababisha mafuriko makubwa kwenye barabara kuu na madaraja katika mji mkuu wa Seoul.
Rais Moon Jae-in anatarajia kuitisha mkutano wa dharura leo Jumanne, siku moja baada ya kutoa wito kwa wakuu wa kitaifa na kikanda kufanya kufanya kinachowezekana ili kuzuia vifo zaidi.