Pata taarifa kuu
MAREKANI

Marekani: CDC yaagiza uvaaji wa barakoa katika maeneo yanayokumbwa na COVID

Maafisa wa afya nchini Marekani wametangaza hatua mpya ya uvaaji wa barakoa kwa watu waliopewa chanjo kamili dhidi ya COVID, wakisema ni bora kuendelea kuvaa barakoa katika maeneo yaliyofungwa katika majimbo ya Marekani ambapo Corona inaendelea kusambaa kwa kasi.

Wakati aina mpya ya kirusi cha Corona, kinacoambukiza zaidi kikiendelea kusambaa nchini Marekani, utafiti unaonyesha kuwa mtu mmoja kuvaa barakoa ni kinga bora.
Wakati aina mpya ya kirusi cha Corona, kinacoambukiza zaidi kikiendelea kusambaa nchini Marekani, utafiti unaonyesha kuwa mtu mmoja kuvaa barakoa ni kinga bora. AFP - KENA BETANCUR
Matangazo ya kibiashara

Wakati wa mkutano na waandishi wa habari, wawakilishi kutoka Vituo vya Udhibiti na Kuzuia Magonjwa nchini Marekani (CDC) wamesema kituo hicho kimeagiza walimu na wanafunzi wote, bila kujali hali yao ya chanjo kuvaa barakoa.

Pia wametoa wito kwa mamlaka husika kushinikiza raia kupata chanjo na kuvaa barako ili kuzuia kuenea zaidi kwa janga la Corona katika maeneo ambapo kiwango cha maambukizi kiko juu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.