Pata taarifa kuu
MAREKANI-AFYA

Marekani: Idara za ujasusi zapitisha nadharia mbili juu ya chimbuko ya COVID-19

Makao makuu ya Upelelezi nchini Marekani imesema kwamba mashirika yake yana nadharia mbili juu ya chanzo cha janga la COVID-19, idara mbili zinaweka mbele nadharia ya kuibuka kwa asili kupitia mawasiliano ya kibinadamu na wanyama wenye virusi vya Corona, idara ya tatu ikitetea nadharia ya ajali inayowezekana ya maabara.

Katika ripoti yao ya kwanza, idara za ujasusi nchini Marekani zilishindwa kupata majibu. Baada ya kutoridhika, Joe Biden amezitaka "kuzidisha juhudi zao" na kwa hivyo amezipa siku 90 kutoa ripoti ya pili yenye ujumbe rasmi wa "kutuleta karibu na hitimisho la mwisho" juu ya hali hizi mbili ambazo White House
Katika ripoti yao ya kwanza, idara za ujasusi nchini Marekani zilishindwa kupata majibu. Baada ya kutoridhika, Joe Biden amezitaka "kuzidisha juhudi zao" na kwa hivyo amezipa siku 90 kutoa ripoti ya pili yenye ujumbe rasmi wa "kutuleta karibu na hitimisho la mwisho" juu ya hali hizi mbili ambazo White House Ted ALJIBE AFP/File
Matangazo ya kibiashara

"Mashiria ya ujasusi ya Marekani hayana uhakika ni wapi, lini, au jinsi virusi vya COVID-19 vilipitishwa mwanzoni, lakini yamekusanya karibu matukio mawili," ofisi ya mkurugenzi wa ujasusi katika ngazi ya kitaifa imesema.

Idara nyingi inaamini kwamba kuna "habari za kutosha kukadiria uwezekano mmoja zaidi kuliko mwingine," imeongeza.

Rais wa Marekani Joe Biden Jumatano aliomba idara za ujasusi za Marekani kumpa ripoti juu ya chimbuko cha janga hilo ndani ya siku 90.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.