BRAZILI
Coronavirus: Brazil yapitisha kizingiti cha vifo 300,000
Brazil imerekodi vifo vipya 2,009 kutokana na COVID-19 kwa siku moja, kulingana na takwimu zilizotolewa Jumatano wiki hii na Wizara ya Afya nchini humo, na kufikidsha jumla ya vifo 300,000.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Karibu visa 90,000 vipya vya maambukizi pia vimegunduliwa katika kipindi cha saa ishirini na nne.
Waziri mpya wa Afya, Marcelo Queiroga, aliahidi Jumatano mchana kwamba serikali itafanya kazi ili kuharakisha kampeni ya chanjo.
Wakati wa mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari, alisema lengo la serikali ilikuwa kutoa dozi milioni moja za chanjo hiyo kila siku.