Pata taarifa kuu
MAREKANI-BIDEN-SIASA

Biden aidhinishwa kuchuana na Donald Trump katika uchaguzi wa urais Marekani

Joe Biden ameteuliwa rasmi na chama chake cha Democratic, kuwania urais wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Novemba kupambana na rais Donald Trump.

Joe Biden, apitishwa kupeperusha bendera ya chama cha Democratic katika uchaguzi wa urais, akiambatana na mkewe Jill, kwenye video iliyorushwa mtandaoni wakati wa Mkutano Mkuu wa chama cha Democratic, Agosti 18, 2020.
Joe Biden, apitishwa kupeperusha bendera ya chama cha Democratic katika uchaguzi wa urais, akiambatana na mkewe Jill, kwenye video iliyorushwa mtandaoni wakati wa Mkutano Mkuu wa chama cha Democratic, Agosti 18, 2020. DEMOCRATIC NATIONAL CONVENTION / AFP
Matangazo ya kibiashara

Wajumbe wa chama hicho kutoka majimbo yote 50 wamekuwa wakikutana kupitia njia ya video kwa sababu ya janga la Corona.

Biden ambaye anatarajiwa kuwahotubia wajumbe hao siku ya Alhamisi, amewashukuru kwa kumwidhinisha yeye pamoha na mgombea mwenza wake Kamala Harris.

Marais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton na Jimmy Carter, walimsifu Biden kuwa mtu mwenye uzoefu na uadilifu wa kuinusuru Marekani iliyoathiriwa vibaya na janga la Corona.

Kongamano hilo la siku nne, mwaka huu linafanyika kwa njia ya vidio kutokana na janga la Covid-19.

Hii ni mara ya tatu kwa Biden kuingia kwenye kinyang'anyiro cha urais huku mwakilishi huyo wa chama cha Democratic akionekana kuwa katika kipindi cha madiliko makubwa ikizingatiwa kwamba kampeni yake ilionekana kuwa katika hatari ya kudidimia mnamo mwezi Februari.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.