Pata taarifa kuu
MAREKANI-TRUMP

Trump amshtumu Obama kuchochea vurugu Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump anasema anaamini kuwa mtangulizi wake Barrack Obama, anachochea maandamano yanayojitokeza kupinga hatua yake ya kutaka wahamiaji kutoka mataifa saba ya Kiislamu wasije Marekani kwa sababu za kiusalama.

Donald Trump amlaumu Rais Barack Obama kwa kuchochea maandamano.
Donald Trump amlaumu Rais Barack Obama kwa kuchochea maandamano. REUTERS/Kevin Lamarque
Matangazo ya kibiashara

Trump amelimbia Shirika la Habari la Fox News kwamba ana imani kuwa Obama anahusika kwa njia moja ama nyingine sababu ni watu wake wanaohusika kwenye maandamano hayo, huku akiongeza kwamba pingamizi dhidi yake ni kwa sababu za kisiasa.

Rais Donald Trump amesema anaamini kuwa Barack Obama ndiye anahusika na maandamano dhidi ya uongozi wa Republican.

Obama hajamjibu Trump kuhusu madai haya.

Bush akosoa maamuzi ya kwanza ya Trump

Rais wa zamani wa Marekani George W. Bush, alifanya mahojiano na kituo cha habari cha NBCna kukosoa maamuzi ya kwanza ya rais wa sasa wa Marekani.

George W. Bush, pamoja na Hillary Clinton, wakati Donald Trump akitawazwa kuwa rais wa Marekani, Januari 20, 2017.
George W. Bush, pamoja na Hillary Clinton, wakati Donald Trump akitawazwa kuwa rais wa Marekani, Januari 20, 2017. Timothy A. CLARY / AFP

Katika kipindi cha miaka minane iliyopita, rais wa zamani alijizuia kumkosoa mrithi wake, Barack Obama. Hata hivyo ameamua kumkosa kwa Rais Donald Trump. Bila hata hivyo kumtaja jina, rais wa zamani wa Marekani amesema kuwa ana imani na vyombo vya habari ambavyo, kwa upande wake, vinadumisha na kuhimiza wananchi kujua misingi ya demokrasia.

Amebaini kinyume na alivyosema Trump, kwamba vyombo vya habari si maadui wa Marekani.

Trump kulihutubia taifa Jumanne hii

Siku arobaini baada ya kuchukua hatamu ya uongozi wa nchi, Donald Trump atalihutubia taifa Jumanne hii, Februari 28 bele ya Bunge na Baraza la Seneti.

Itakua ni mara ya kwanza Rais Donald trump kulihutubia taifa toka kutawazwa kwake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.