Pata taarifa kuu
DRC-EBOLA-AFYA

WHO: Ebola imeua watu 122 mashariki mwa DRC

Idadi ya watu waliopoteza maisha Mashariki mwa DRC kutokana na ugonjwa wa Ebola imeongezeka na kufikia 122, kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) ya tarehe 9 Oktoba 2018.

Kituo kinachotua huduma kwa wagonjwa wa Ebola (CTE) Mangina, Kivu Kaskazini, DRC.
Kituo kinachotua huduma kwa wagonjwa wa Ebola (CTE) Mangina, Kivu Kaskazini, DRC. Florence Morice/RFI
Matangazo ya kibiashara

Watoto watatu ni miongoni mwa watu waliyopoteza maisha hivi karibuni, kwa mujibu wa maafisa wa Wizara ya afya.

Inaripotiwa kuwa, watu wengine sita walioppoteza maisha ni wakaazini wa Beni, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Uganda.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema imewapa chanjo watu 15,000 katika jimbo la Kivu Kaskazini ili kuepusha maambukizi zaidi.

Wakaazi wa Jimbo la Kivu Kaskazini wametakiwa kuendelea kushirikiana na maafisa wa afya kwa kuwafikisha katika vituo vya afya wale wote wanaoshukwia kuwa na dalili za Ebola.

Mbali na hayo, maafisa wa usalama nchini humo wameanza kuwasindikiza wagonjwa baada ya kuongezeka kwa visa vya utovu wa usalama Wilayani Beni.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.