Pata taarifa kuu

Afrika Kusini: Majaji kuamua iwapo Zuma atawania urais au la

Nairobi – Majaji nchini Afrika Kusini wanatarajiwa kutoa uamuzi iwapo rais wa zamani Jacob Zuma ataruhusiwa kugombea uchaguzi wa mwezi Mei au la, baada ya kuzuiwa na Tume ya Uchaguzi.

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma.
Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma. AP - Themba Hadebe
Matangazo ya kibiashara

Zuma ambaye alihamia chama cha uMkhonto weSizwe kutoka chama tawala cha ANC, alikosimamishwa uanachama, alikataa rufaa kupinga uamuzi wa Tume ya Uchaguzi.

Mwezi uliopita, Maafisa wa Tume ya Uchaguzi walieleza kuwa walimzuia Zuma kwa sababu alipatikana na hatia na Mahakama na kuhukumiwa jela, kwa kuidharau Mahakama.

Hata hivyo, Mawakili wake wamedai kuwa hukumu hiyo haimwondolei uhuru wake wa kugomegea uongozi wa nchi yake.

Jacob Zuma, anasema kuwa raia wa Afrika Kusini ndio wenye kuamua iwapo atawania urais au la.
Jacob Zuma, anasema kuwa raia wa Afrika Kusini ndio wenye kuamua iwapo atawania urais au la. © Kim Ludbrook / AP

Jumatatu ya wiki hii, Zuma mwenye umri wa miaka 81 akiwa  Mahakamani jijini Johannesburg kusikiliza rufaa yake, aliwaambia wafausi wake nje ya Mahakama kuwa, iwapo wananchi wanataka awe rais hakuna anayeweza kumzuia.

Afrika Kusini inatarajiwa kuandaa uchaguzi mkuu tarehe 29 mwezi Mei, unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali katika historia ya nchi hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.