SADC inataka kuimarisha wanajeshi wake mashariki mwa DRC
Wakuu wa vikosi vya ulinzi vya nchi nne wanachama wa SADC na Burundi wanatangaza azma yao ya kuweka amani katika eneo lililoathiriwa na uasi wa M23. Waliyasema hayo siku ya Jumamosi Machi 2 mwishoni mwa misheni ya siku tatu wanakwenda Goma (Kivu Kaskazini).
Imechapishwa:
Kulingana na Radio OKAPI, viongozi Wakuu watano kutoka nchi zifuatazo walikutana siku ya Alhamisi na Ijumaa kutathmini operesheni za pamoja zinazoendelea ndani ya mfumo wa ujumbe wa SADC nchini DRC:
Afrika Kusini
Malawi
Tanzania
DRC
Burundi
Mwishoni mwa siku mbili za kazi, viongozi wa majeshi wa nchi hizi tano waliahidi, pamoja na mambo mengine, kuwatia nguvu wanajeshi wa ujumbe wa SADC unaoshirikiana na wanajeshi wa Burundi na FARDC dhidi ya uasi wa M23.
Pia walitekeleza mikakati ya kuweka amani katika eneo hilo. Hivi ndivyo msemaji wa jeshi la FARDC, Meja Jenerali Sylvain Ekenge, alitangaza kwa waandishi wa habari mwishoni mwa mikutano hii:
"Ilikuwa ni suala la kutathmini mabadiliko ya utendaji kazi mashinani na kuboresha mikakati ya kuziimarisha. Ili kuangalia hali hiyo, walikwenda Mubambiro. Uwepo wao huko Goma ni ishara kubwa ambayo inatangaza dhamira na nia njema ya SADC na Burundi pamoja na DRC, kwa ajili ya kurejesha amani katika sehemu yake ya mashariki.
Ujumbe wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (SAMIDRC) ulitumwa Desemba 15, 2023, "kwa nia ya kuunga mkono serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika juhudi zake za kurejesha amani na utulivu mashariki mwa DRC.