Pata taarifa kuu

Nchini Comoro, wahamiaji wasimamishwa kazi baada ya kusitishwa kwa haki za ardhi Mayotte

Hivi majuzi Paris ilitangaza hatua tata inayolenga kusitisha haki za ardhi katika kisiwa cha Ufaransa cha Mayotte katika jaribio la kuzuia wimbi la wahamiaji hasa kutoka nchi jirani ya Comoro.

Mji wa Mutsamudu ulioko kwenye kisiwa cha Anjouan katika visiwa vya Comoro (picha ya kielelezo).
Mji wa Mutsamudu ulioko kwenye kisiwa cha Anjouan katika visiwa vya Comoro (picha ya kielelezo). © Wikimedia Commons CC-BY 2.0 David Stanley
Matangazo ya kibiashara

 

Kijiji hiki kilicho mwisho wa ardhi ya Comoro ndicho kituo cha mwisho kwa maelfu ya wahamiaji wa Kiafrika wanaojaribu kufikia eneo la Ufaransa la Mayotte kwa siri. Lakini siku hizi, boti zotz zimefungwa: Ufaransa imetangaza mkondo mpya wa kukabiliana na uhamiaji haramu.

Mayotte, katika Bahari ya Hindi, ina wakazi 310,000, kulingana na takwimu rasmi ambazo pengine hazijakadiriwa kwa kiasi kikubwa, ikiwa ni pamoja na wahamiaji 48% kutoka Comoro na nchi nyingine za Afrika.

Kikiwa kwenye milima ya kisiwa cha Comoro cha Anjouan, kijiji cha Kangani ni mkono wa bahari na baadhi ya kilomita 70 kutoka idara ya 101 ya Ufaransa. Kisiwa hicho chenye shule na hospitali zake vnavyoto huduma kwa watu wengi wa Comoro, hata kama eneo hilo ndilo maskini zaidi nchini Ufaransa.

Familia zinazotafuta maisha bora, lakini pia sigara na mifugo kawaida hupakiwa mara kadhaa kwa siku kwenye boti za mbao zilizozoeleka kwa uvuvi na zinazoitwa "kwassa-kwassas". Uchumi mzima wa kijiji unazunguka katika njia hii hatari na biashara hufanywa katika noti za euro.

Lakini kwa wiki kadhaa, wakaazi waliokasirishwa na ukosefu wa usalama na uhamiaji haramu wamekuwa wakiweka vizuizi vya barabarani huko Mayotte, na Paris hivi karibuni ilitangaza hatua tata inayolenga kuondoa haki za ardhi katika kisiwa hicho ili kukomesha wimbi la wahamiaji. Tangu wakati huo, mitaa yenye kupindapinda ya Kangani imeingia katika hali ya utulivu.

"Vizuizi vinatuathiri sote, hakuna tena boti za kwassa-kwassa tena zinaoondoka kwa kusubiri kurejea kwa hali ya kawaida," analalamika Chadhuli Tafsir, kijana wa miaka thelathini kutoka Kangani. "Kukomeshwa kwa haki za ardhi ni wazo mbaya kwa kila mtu," anasisitiza, akiendelea na mjadala mkali na wanaume waliokusanyika katika uwanja wa kijiji.

Wakati mwingine unapaswa kusubiri siku kadhaa ili kujaribu kuvuka kwenye bahari. Boti hizo hupinduka mara kwa mara na wahamiaji wengi wametoweka baharini kati ya Comoro na Ufaransa. Labda maelfu, hakuna takwimu rasmi.

"Hakuna mtu angeweza kuchukua hatari ya kwenda Mayotte lakini hatuna chaguo. Kusafiri baharini ni chaguo letu pekee," anasema Jeansi kwa sauti ya kukata tamaa, ambaye anasubiri safari ya pili ya meli kuelekea Ufaransa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.