Pata taarifa kuu

Uchaguzi wa urais unafanyika nchini Madagascar

Nairobi – Raia wa Madagascar leo hii wanashiriki uchaguzi wa urais ambao umesusiwa na wagombea wengi wa upinzani huku kukiwa na hali ya wasiwasi nchini humo.

Hapo jana polisi waliweka kafyu katika mji wa Antananarivo wakidai njama ya kuvuruga uchaguzi huo
Hapo jana polisi waliweka kafyu katika mji wa Antananarivo wakidai njama ya kuvuruga uchaguzi huo © Photos AFP - Montage RFI
Matangazo ya kibiashara

Rais Andry Rajoelina ni miongoni mwa wagombea 13 wanaowania kiti cha urais huku wagombea 10  wa upinzani wakiwa wamekataa kushiriki na baadala yake kuwataka raia kususia zoezi hilo ,wakidai kumekuwa na mikakati ya kupendelea utawala uliopo madarakani.

Tangu oktoba mwaka huu, viongozi wa upinzani wakiwemo marais wawili wa zamani, wamekuwa wakifanya maandamano kupinga kila walichodai ni kutokuwepo kwa suala la uhuru na uwazi katika mikakati ya kuandaa uchaguzi huo.

Uchaguzi umesusiwa na baadhi ya wanasiasa wa upinzani wanaodai kuwa hautakuwa wa huru na haki
Uchaguzi umesusiwa na baadhi ya wanasiasa wa upinzani wanaodai kuwa hautakuwa wa huru na haki AFP - RIJASOLO

Hapo jana polisi waliweka kafyu katika mji wa Antananarivo wakidai njama ya kuvuruga uchaguzi huo.

Rais  Rajoelina aliingia madarakani mwaka 2009 baada ya mapinduzi ila hakuwania muhula uliofuata na akarejea  madarakani  mwaka 2018 na ameeleza matumaini makubwa ya kushinda uchaguzi huu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.