Pata taarifa kuu

Mwanajeshi wa zamani wa Liberia awekwa kizuizini kabla ya kesi nchini Ufaransa

Mwanajeshi wa zamani wa Liberia amewekwa kizuizini siku ya Jumaane Septemba 25 kabla ya kusikilizwa kwa kesi yake siku ya Jumanne hii, na Mahakama ya Rufaa ya Paris. Anashutumiwa kwa uhalifu dhidi ya binadamu wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Liberia katika miaka ya 1990.

Picha iliyopigwa Oktoba 11, 2017 inaonyesha  jiji la Monrovia, mji mkuu wa Liberia.
Picha iliyopigwa Oktoba 11, 2017 inaonyesha jiji la Monrovia, mji mkuu wa Liberia. AFP - ISSOUF SANOGO
Matangazo ya kibiashara

Mshtakiwa huyo ambaye ameishi Ufaransa kwa miaka 20 tayari alikuwa amefunguliwa mashtaka Septemba 13 kabla ya kuwekwa chini ya uangalizi wa mahakama. Uamuzi huu wa kisheria ulichukuliwa dhidi ya ushauri wa ofisi ya mwendesha mashtaka wa kitaifa wa kupambana na ugaidi, ambaye alikata rufaa na hatimaye kupata kizuizini cha muda.

Hatua hizi za kisheria zinafuatia malalamiko yaliyowasilishwa na Civitas Maxima. Tangu 2012, shirika hili lisilo la kiserikali limekuwa likiandika na shirika la Liberia la Global Justice and Research Project (GJRP) uhalifu uliofanywa wakati wa vita viwili vya wenyewe kwa wenyewe, ambavyo viliitikisa Liberia, kuanzia 1989 hadi 1997, kisha kutoka 1999 hadi 2003.

Kulingana na Civitas Maxima, jina la mshtakiwa ni Saturday. Anasemekana kuwa mmoja wa makamanda wa NPFL wakiongozwa na rais wa zamani Charles Taylor wakati wa Charles Taylor alipokuwa kiongozi wa waasi wakati wa vita vya kwanza vya Liberia. Kulingana na uchunguzi wa Tume ya Ukweli na Maridhiano ya Liberia, wanamgambo wa Taylor wanahusika na visa 64,000 vya ukiukaji wa haki za binadamu. Mshtakiwa huyo Saturday anahusishwa kwa kuwajibika katika vitendo kadhaa vya uhalifu dhidi ya binadamu vilivyofanywa wakati wa mzozo huo ambao unasemekana ulisababisha vifo vya watu kati ya 150,000 na 250,000.

Hii ni kesi ya kumi na moja ambayo Civitas imewasilisha mbele ya mahakama nje ya nchi, ingawa hakuna kesi zilizosikilizwa nchini Liberia. Mwaka jana, kamanda wa zamani wa waasi Kunti Kamara alihukumiwa kifungo cha maisha jela nchini Ufaransa kwa kuhusika na uhalifu dhidi ya binadamu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.