Pata taarifa kuu

Somaliland yapuuza mapendekezo ya rais wa Uganda kuhusu mazungumzo ya amani

Somaliland imesema haina mpango wa kufanya mazungumzo kuhusu mipango ya kujadili suala ya amani, hatua inayokuja baada ya rais wa Uganda Yoweri Museveni, kujitolea kuwa mpatanishi kati ya eneo hilo ambalo limejitenga na serikali ya shirikisho ya Somalia.

Somaliland imesema haina mpango wa kufanya mazungumzo kuhusu mipango ya kujadili suala ya amani
Somaliland imesema haina mpango wa kufanya mazungumzo kuhusu mipango ya kujadili suala ya amani © RFI
Matangazo ya kibiashara

Jumapili ya wiki iliyopita, rais Museveni, alisema amekubali kuchukua nafasi ya mratibu wa amani kati ya pande hizo mbili baada yake kukutana na mjumbe wa serikali ya Somaliland jijini Entebbe Uganda.

Wakati wa mazungumzo hayo, rais Museveni alisema haungi mkono mpango wa eneo la Somaliland kujitenga akisema halikuwa suala bora.

Kwa upande mwengine, uanchama wa Uganda na Jamhuri ya Afrika ya Kati ulisitishwa kutoka Agoa kwa madai ya ukiukaji wa haki za binadamu
Kwa upande mwengine, uanchama wa Uganda na Jamhuri ya Afrika ya Kati ulisitishwa kutoka Agoa kwa madai ya ukiukaji wa haki za binadamu AP - Bebeto Matthews

Katika taarifa yake, wizara ya mambo ya kigeni ya Somaliland ilisema mazungumzo ya aina yoyote na serikali ya Mogadishu, hayatajadili suala ya umoja bali yanapaswa kujadili namna pande hizo mbili zinaweza kusonga mbele kibnafsi.

Somaliland ilitangaza kuwa huru kutoka kwa Somalia mwaka wa 1991 na imekuwa ikitaka kutambuliwa kama nchi huru bila ya mafanikio.

Mazungumzo kati ya pande hizo mbili yamekuwa yakifanyika kwa miaka kadhaa sasa, suala ya uongozi wa anga, uhuru wa eneo la Somaliland yakiwa mojawapo ya mambo yanayozungumziwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.