Pata taarifa kuu

Nchi za Magharibi zaahidi kusaidia mataifa ya Afrika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Mkutano wa kwanza wa ngazi ya juu wa hali ya hewa barani Afrika umeingia siku yake ya pili hii leo katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, huku wajumbe wakilenga kuweka msimamo mmoja kabla ya mikutano ijayo ya kimataifa na kujadili jinsi ya kufadhili vipaumbele vya mazingira katika bara hilo.

Ufaransa  na mataifa mengine ya magharibi yaahidi kutoa msaada kwa Afrika kufuatia mabadiliko ya tabia nchi.
Ufaransa na mataifa mengine ya magharibi yaahidi kutoa msaada kwa Afrika kufuatia mabadiliko ya tabia nchi. AP - Sarah Meyssonnier
Matangazo ya kibiashara

Rais William Ruto,mwenyeji wa mkutano huo na ambaye pia ndiye mwenyekiti wa kamati ya viongozi wa Afrika juu ya mabadiliko ya tabia nchi, amesema kuwa wakati umefika kwa Afrika kuhusishwa kikamilifu na kusikilizwa kama mmoja wa wadau wenye suluhisho.

 "Ni mda viongozi wawe wazi,wakweli  na waweke suluhu zote mezani ili kujiendeleza"amesema Rais William Ruto.

Wakati huo huo Ruto ametoa wito kwa vijana barani Afrika kujiweka mstari wa mbele katika kuokoa bara hili kutokana na  athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Rais wa Kenya William Ruto akihutubia katika kongamno la Afrika kuhusu Mabadiliko ya tabia nchi
Rais wa Kenya William Ruto akihutubia katika kongamno la Afrika kuhusu Mabadiliko ya tabia nchi AP - Khalil Senosi

Kauli hii imeendana na wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyesema kuwa vijana wakipewa fursa ya kuchangia, na kuwezeshwa kwa uwekezaji, suluhisho itapatikana kwa haraka.

Kwenye uhusiano na kongamano hilo Waziri wa Ufaransa, Chrysoula Zacharopoulou  , anayeshughulika na masuala ya maendeleo ya kimataifa na Francophonie, katika ziara yake katika mtaa wa mabanda wa Mukuru ya Njenga, amesema nchi hiyo itashirikiana na mashirika mengine ya Kimataifa kusaidia kuimarisha mazingira miongoni mwa jamii masikini.

00:16

Chrysoula Zacharopoulou

Zacharopoulou , aliambatana na aliyekuwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban ki Moon ambaye amesema, nchi za Afrika zinapaswa kujisimamia kwenye mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.

 

00:18

Ban ki Moon

Katika hatua nyingine, Ufaransa imesema itatoa msaada wa Euro millioni moja ili kuwawezesha wanafunzi kupata chakula katika mitaa duni, kama Kibera jijini Nairobi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.