Cyril Ramaphosa na Joe Biden wakubaliana kushirikiana katika masuala mbalimali
Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa na mwenyeji wake rais wa Marekani Joe Biden, wamekutana na kukubaliana kushirikiana kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo afya, usalama na mabadiliko ya tabia nchi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Hata hivyo, rais Ramaphosa amekosoa mataifa ya Magharibi kuyatesa yale ya Afrika kwa kuendelea kushirikiana na Urusi, licha ya kuivamia Ukraine.
Kuhusu usalama nchini Msumbiji, rais Ramaphosa amesema ameomba msaada wa Marekani ili kuyashinda makundi ya kijihadi.
Tumajadiliana kuhusu utovu wa usalama nchini Msumbiji, na tumeiomba Marekani isaidie kwa sababu Afrika Kusini ipo kwenye hatari ya kushalmbliwa;. Tnahitaji fedha, kwa sasa Afrika Kusini imetuma idadi kubwa ya wanajeshi wake mbali na Rwanda, na hili limepokelewa vema na majadiliano yatanyika.
.