Pata taarifa kuu

Takriban watu 3 wafariki katika ajali ya bwawa la uchimbaji madini nchini Afrika Kusini

Watu arobaini wamepelekwa katika hospitali mbalimbali baada ya bwawa la uchimbaji madini kuporomoka nchini Afrika Kusini; sababu za tukio hilo bado hazijajulikana.

Mfanyakazi wa kampuni ya Bathopele, katika mgodi wa Afrika Kusini wa Runstenburg.
Mfanyakazi wa kampuni ya Bathopele, katika mgodi wa Afrika Kusini wa Runstenburg. AFP PHOTO / MUJAHID SAFODIEN
Matangazo ya kibiashara

Takriban watu watatu wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya bwawa la kuchimba madini kuporomoka na kusababisha mafuriko na kusomba nyumba katikati mwa Afrika Kusini, maafisa wamesema siku ya Jumapili.

Picha za televisheni zinaonyesha mto wa matope na maji yakitiririka kutoka mgodini hadi katika eneo la makazi la karibu, ambalo limeshika barabara na kusomba nyumba huko Jagersfontein, mji ulio umbali wa kilomita 100 kusini magharibi mwa Bloemfontein, mji mkuu wa Mkoa wa Free State.

"Bwawa la uchimbaji madini liliporomoka na kusomba nyumba na magari," Palesa Chubisi, msemaji wa serikali ya mkoa, amesema katika taarifa. "Miili mitatu imepatikana."

Watu 40, akiwemo mama mjamzito, wamepelekwa katika hospitali za mitaa, wanne kati yao wakiwa wamevunjika miguu na mikono na wengine wakiwa na michubuko na hypothermia, Chubisi ameongeza.

Kulingana na shirika la kitaifa la umeme la Eskom, Jagersfontein pia haina umeme kwa sababu moja ya vituo vyake vya umeme "vimejaa matope".

"Kutokana na hali ya sasa katika eneo la Jagersfontein na kutofikiwa kwa kituo hiki, haiwezekani kukadiria ni lini umeme utarejeshwa au kubaini ukubwa wa uharibifu," Eskom imesema katika taarifa.

Mamlaka zilikuwa zikiwahamisha wakaazi wa maeneo yaliyoathiriwa, ambako nyumba nyingi zilisombwa na maji, hadi kwenye mashamba ya karibu, huku shughuli za utafutaji na uokoaji zikiendelea siku ya Jumapili.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.