Viongozi wa SADC wakutana kujadili masuala mbalimbali katika nchi zao
Viongozi kutoka Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Kusini mwa Afrika SADC wanakutana leo na kesho jijini Kinshasa, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kujadili masuala mbalimbali.
Imechapishwa:
Wakuu wa nchi wanaokutana kwenye mkutano huu wa 42, wanajadiliana kuhusu namna ya kuimarisha ukuaji wa viwanda, kilimo na masuala ya madini katika nchi hizo.
Mbali na masuala ya kiuchumi, DRC ambayo ni mwenyeji wa mkutano huu, inatarajiwa kutumia mkutano huu kutafuta msaada wa kurejesha amani katika eneo la Mashariki ambalo limeendelea kukumbwa na utovu wa usalama.
Mkutano mkuu hufanyika kila mwaka, kuwaleta pamoja, viongozi kutoka nchi 16 kujadili, masuala mbalimbali yanayoikumba Jumuiya hiyo.