Pata taarifa kuu

Tunisia: Maandamano dhidi ya rais Kaïs Saïed yafanyika chini ya uangalizi mkubwa

Maandamano mapya yamefanyika huko Tunis, Jumapili hii, Oktoba 10. Maelfu ya wfuasi wa uapinzani wa rais wa Tunisia Kaïs Saïed walimiminika mitaani wakidai rais huyo ajiuzulu.

Waandamanaji wakati wa mkutano ya kumpinga rais wa Tunisia Saïed Oktoba 10 huko Tunis.
Waandamanaji wakati wa mkutano ya kumpinga rais wa Tunisia Saïed Oktoba 10 huko Tunis. AFP - FETHI BELAID
Matangazo ya kibiashara

Hata kabla ya kuwasili kwenye mtaa wa Bourguiba, eneo la maandamano dhidi ya Rais Saïed, maelfu ya maafisa wa polisi walikuwa wamezingira eneo hilo. Maandamano ya wapinzani wa rais yamefanyika chini ya uangalizi mkubwa.

Mamlaka ilikuwa imepiga marufuku ya maandamano kufanyika katika baadhi ya mitaa, pia marufuku kwa waandishi wa habari kukaribia maandamano hayo. Maafisa wa polisi waliokuwa wamepiga kambi karibu na eneo la maandalano waliwataka waandamanaji kurudi nyuma.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.